GLOBALWISE SOFTNET & GRAPHIC DESIGNER: Mdee awalipua Mwinyi, Mkapa

Monday, August 15, 2011

Mdee awalipua Mwinyi, Mkapa


VIGOGO wa CCM wakiwamo Marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa wamelipuliwa bungeni jana wakituhumiwa kuhodhi maeneo makubwa ya ardhi mkoani Morogoro huku wakishindwa kuyaendeleza.

Katika orodha hiyo ya waliolipuliwa wamo pia Mawaziri Wakuu wastaafu, Frederick Sumaye na John Malecela, Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula, aliyekuwa Naibu wake (Tanzania Bara), Hassan Ngwilizi na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Nawab Mulla.

Tuhuma hizo zilitolewa bungeni Mjini Dodoma na Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee wakati akisoma bajeti mbadala ya upinzani kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka 2011/12.

Mdee alisema hali hiyo inawanyima fursa wananchi wa kawaida kumiliki maeneo kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuongeza kwamba vigogo hao kwa kutumia nafasi zao waliwanyang’anya wananchi ardhi hiyo na kujimilikisha wenyewe lakini kwa sehemu kubwa wameshindwa kuyaendeleza.

“Mheshimiwa Spika, matatizo ya ardhi kwa wakubwa kunyang’anya wanyonge yameikumba pia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero (Morogoro), ambako mgogoro huu unakumba shamba namba 299 iliyokuwa NARCO Ranches lenye ukubwa wa hekta 49,981,” alisema na kuongeza:

No comments: